Monday, 10 August 2015

NAKUJA NA ZAWADI



NAKUJA NA ZAWADI
Naondoka mimi naenda kwa Baba,
Nipeleke hiki nilichokipata,
Japo kidogo, sitaona haya,  
Nimeamua, sitarudi nyuma
Nakuja polepole Baba,
Nakuja na zawadi yangu
Naleta mbele zako
Ili nitoe shukurani *2
  1. Natembea mimi mwendo wa madaha,
    Nakanyaga chini kwa maringo tele,
    Naelekea altare ya Bwana,
    Nimkabidhi nilichojaliwa.
  2. Nimechangamka ninashangilia,
    Napiga kelele, kelele za shangwe
    Nachezacheza, najongea kwako,
    Ee Mungu Baba Nipokee mimi.
  3. Nafsi yangu mimi naileta kwako,
    Mkate divai, pia ninaleta
    Uigeuze mwili na damuyo,
    Chakula chetu, tunaosafiri
  4. Mavuno shambani mimi nimevuna,
    Mifukoni fedha nimekabidhiwa,
    Mimi ni nani, nisikushukuru,
    Baba nasema asante kwa yote.

No comments:

Post a Comment