Monday, 17 August 2015

MWILI WA BWANA YESU

MWILI WA BWANA YESU
  1. Mwili wa Bwana Yesu, chakula cha Mbingu
    Ni chakula cha roho, chenye uzima
    Hima uwe nasi ee Bwana Yesu
    Ukatushibishe chakula bora
    Ni chakula cha roho, chenye uzima *2
  2. Yesu alituambia, Yeye ni chakula
    Ni chakula cha roho, chenye uzima
    Sote twaamini, ni mwili wake
    Pia twaamini ni damu yake
    Ni chakula cha roho, chenye uzima *2
  3. Yesu alituambia, kuwa tumpokee
    Ni chakula cha roho, chenye uzima
    Ee Bwana mkombozi tunakuomba
    Kwa chakula hiki tuinamie
    Ni chakula cha roho, chenye uzima *2
  4. Hii ndiyo karamu, aliyotuachia
    Ni chakula cha roho, chenye uzima
    Alaye mwili na kunywa damu
    Ana uzima wa siku zote
    Ni chakula cha roho, chenye uzima *2

No comments:

Post a Comment