MISA
AMECEA - UTUKUFU
Utukufu kwa Mungu juu mbinguni
Na amani kote duniani
(Kwa watu) wenye mapenzi mema
|s/a| Tunakusifu Baba, tunakuheshimu,
Twakuabudu sisi tunakutukuza
|t/b| Kusifu tunakusifu, heshimu,
Twakuabudu abudu tunakutukuza
Na amani kote duniani
(Kwa watu) wenye mapenzi mema
|s/a| Tunakusifu Baba, tunakuheshimu,
Twakuabudu sisi tunakutukuza
|t/b| Kusifu tunakusifu, heshimu,
Twakuabudu abudu tunakutukuza
Twakushukuru Mungu kwa ‘tukufu
Wako mkuu ewe Mungu mfalme
(Ee Baba) wa Mbingu Baba yetu
Wako mkuu ewe Mungu mfalme
(Ee Baba) wa Mbingu Baba yetu
Bwana wetu mwokozi Yesu Kristu
Mwana wa pekee wake Mungu
(Uliye) Mwanakondoo wa Mungu
Mwana wa pekee wake Mungu
(Uliye) Mwanakondoo wa Mungu
Unayeziondoa dhambi zote
Za dunia utuhurumie
(Pokea) pokea ombi letu
Za dunia utuhurumie
(Pokea) pokea ombi letu
Wewe unayeketi kuume
Kwake Baba utuhurumie
(Sikia) sikia ombi letu
Kwake Baba utuhurumie
(Sikia) sikia ombi letu
Kwani pekee yako ndiwe Bwana
Pekee yako mkuu na mkombozi
(Pekee) pekee Yesu Kristu
Pekee yako mkuu na mkombozi
(Pekee) pekee Yesu Kristu
Kwa umoja wa Roho mtakatifu
Ndani yake Baba watukuzwa
(Ee Yesu) milele na milele
Ndani yake Baba watukuzwa
(Ee Yesu) milele na milele
No comments:
Post a Comment